Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Tuesday, June 25, 2013

Twonane Milele

1. Nyimbo na tuziimbe tena
    Za alivyotupenda mbele;
    Kwa damu ya thamani sana!
    Mbinguni hwonana milele.
 
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.
 
2. Hupozwa kila aoshwaye
    Kwa damu ya kondoo yule;
    Ataishi afurahiye
    Vya Yesu Mbinguni milele.
 
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.
 
3. Hata sasa hufurahia
    Tamu yake mapenzi yale,
    Je, kwake tukifikilia,
    Kutofarakana milele?
 
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.
 
4. Twende mbele kwa jina lake
    Hata aje Mwokozi yule,
    Atatukaribisha kwake,
    Tutawale naye milele.
 
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.
 
5. Sauti zetu tuinue
    Kumsifu Mwokozi yule,
    Ili watu wote wajue
    Wokovu u kwake milele.
 
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.

No comments:

Post a Comment