Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Friday, June 14, 2013

Ni Salama Rohoni Mwangu

1. Nionapo amani kama shwari,
    Ama nionapo shida;
    Kwa mambo yote umenijulisha
    Ni salama rohoni mwangu.
 
         Salama rohoni,
         Ni salama rohoni mwangu.
 
2. Ingawa Shetani atanitesa,
    Nitajipa moyo kwani
    Kristo ameona unyonge wangu,
    Amekufa kwa roho yangu.
 
         Salama rohoni,
         Ni salama rohoni mwangu.
 
3. Dhambi zangu zote, wala si nusu,
    Zimewekwa Msalabani;
    Wala sichukui laana yake,
    Ni salama rohoni mwangu.
 
         Salama rohoni,
         Ni salama rohoni mwangu.
 
4. Ee Bwana himiza siku ya kuja,
    Panda itakapolia;
    Utakaposhuka sitaogopa -
    Ni salama rohoni mwangu.
 
         Salama rohoni,
         Ni salama rohoni mwangu.

No comments:

Post a Comment