Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Wednesday, June 19, 2013

Liko Lango Moja Wazi

1. Liko lango moja wazi,
    Ni lango la Mbinguni;
    Na wote waingiao
    Watapata nafasi.
 
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango
La Mbinguni ni wazi.
 
2. Yesu ndiye lango hili,
    Hata sasa ni wazi,
    Kwa wakubwa na wadogo,
    Tajiri na maskini.
 
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango
La Mbinguni ni wazi.
 
3. Hili ni lango la raha,
    Ni lango la rehema;
    Kila mtu apitaye
    Hana majonzi tena.
 
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango
La Mbinguni ni wazi.
 
4. Tukipita lango hili
    Tutatua mizigo
    Tuliyochukua kwanza,
    Tutavikwa uzima.
 
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango
La Mbinguni ni wazi.
 
5. Hima ndugu tuingie
    Lango halijafungwa,
    Likifungwa mara moja
    Halitafunguliwa.
 
Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango
La Mbinguni ni wazi.

No comments:

Post a Comment