Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Tuesday, June 18, 2013

Kazi Yangu Ikiisha

1. Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka;
    Na kuvaa kutokuharibika,
    Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni;
    Atakuwa wa kwanza kunilaki.
 
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
 
2. Furaha nitapata nikiona makao
    Bwana aliyotuandalia;
    Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
    Vilivyonipa pahali mbinguni.
 
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
 
3. Nao waliokufa katika Bwana Yesu,
    Nitawaona tena huko juu;
    Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni,
    Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
 
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.
 
4. Milangoni mwa mji Bwana atanipisha,
    Pasipo machozi wala huzuni.
    Nitauimba wimbo wa milele; lakini
    Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
 
Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso;
Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari.

No comments:

Post a Comment