Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Wednesday, June 12, 2013

Twasoma Ni Njema Sana

1. Twasoma, ni njema sana
    Mbinguni, kwa Bwana;
    Twasoma, dhambi hapana,
    Mbinguni, kwa Bwana;
    Malaika wema wako,
    Vinanda vizuri viko,
    Na majumba tele yako,
    Mbinguni kwa Bwana.

2. Siku zote ni mchana,
    Ni nchi ya raha;
    Wala machozi hapana,
    Ni nchi ya raha;
    Walioko wauona
    Uso wa Mwokozi, tena
    Jua jingine hapana,
    Ni nchi ya raha.

3. Nyama na vitu viovu
    Havimo kabisa;
    Kifo nacho, na ubovu,
    Havimo kabisa,
    Ni watakatifu wote,
    Wameoshwa dhambi zote;
    Wasiosafiwa wote
    Hawamo kabisa.

4. Tuna dhambi pia sote,
    Mwokozi akafa;
    Kwake tutaoshwa zote,
    Mwokozi akafa;
    Kwake twapata wokovu,
    Tutawona utukufu;
    Mbinguni tutamsifu;
    Mwokozi akafa.

5. Baba, mama, ndugu zetu,
    Twendeni kwa Bwana;
    Huku chini siko kwetu,
    Twendeni kwa Bwana;
    Tusishikwe na dunia,
    Na dhambi kutulemea,
    Tutupe vya chini pia,
    Twendeni kwa Bwana.

No comments:

Post a Comment