Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Thursday, June 13, 2013

Twende Kwa Yesu

1. Twende kwa Yesu mimi nawe,
    Njia atwonya tuijue
    Imo Chuoni; na Mwenyewe,
    Hapa asema, Njoo!
 
         Na furaha tutaiona,
         Mioyo ikitakata sana,
         Kwako, Mwokozi, kuonana,
         Na milele kukaa.
 
2. "Wana na waje" atwambia,
    Furahini mkisikia,
    Ndiye mfalme wetu pia,
    Na tumtii, Njoo.
 
        Na furaha tutaiona,
        Mioyo ikitakata sana,
        Kwako, Mwokozi, kuonana,
        Na milele kukaa.
 
3. Wangojeani? Leo yupo;
    Sikiza sana asemapo;
    Huruma zake zikwitapo,
    Ewe kijana, Njoo.
 
       Na furaha tutaiona,
       Mioyo ikitakata sana,
       Kwako, Mwokozi, kuonana,
       Na milele kukaa.

1 comment: