Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Monday, June 24, 2013

Kujishusha


Matatizo mengi katika jamii yetu yanatokana na kila mmoja kujiinua, kutaka kutambulika (umaarufu), pia kwasababu hatuna roho ya kujishusha.
Migogoro mingi katika familia ni kwa kuwa kina mama wanataka kuwa nafasi sawa na kina baba, wakijua kwamba wana uwezo wa kumudu majukumu, zaidi mpango wa haki sawa kwa wote umebadilisha kabisa maadili katika jamii nzima.
Mwanzo 3:16
Matatizo mengi katika maeneo ya kazi pia yanatokana na kutojishusha kwa mfanyakazi au mwajiriwa ambaye anaona anajua zaidi kuliko mkubwa wake, ama ni haki yake. Nakumbuka wakati mmoja mama yangu aliniambia kuwa “mwanangu mkubwa hakosei”, na si kwamba mama alimaanisha kuwa hakika mkubwa hakosei ila yampasa mdogo kushuka.
Mwanzo 39:11 – 19
Yusufu alikuwa na kila sababu ya kujitetea na kupignia haki yake, lakini aliamua kujishusha akiamini kwamba ndivyo inavyompasa kuenenda na kufanya, na hakika alimuona Mungu akimpigania na kumuinua hata alipokuwa gerezani.
Bwana wetu Yesu alijishusha sana hata kufikia mauti ya msalaba. Ingawa Yeye ni mfalme wa wafalme, lakini hakuishi katika jumba la kifaari, zaidi alipiga kambi na wanafunzi wake popote. Lakini pia, hata alipokamatwa, akateswa sana na kutemewa mate na kuishia msalabani, alisema “Baba uwasamehe kwa kuwa hawajui walitendalo”. Lakini, katika kujishusha kote huku ndipo tumepata wokovu mkuu na ulio wa thamani sana leo hii.
Mathayo 8:20 | Luka 23:34
Yakobo 4:10
Mtu anayejishusha siku zote Mungu humuinua sana. Zaidi, kujishusha ni kutohesabu vingapi tunapoteza ila kuachia kusudi la Mungu liweze kutimia katika maisha yetu. Mwizi anapokuja kuiba hazina yako ambayo Mungu alikusudia iwe yako, ataambulia kuchuma laana, lakini wewe utamuona Mungu akikubariki kwa hazina zaidi.
Warumi 12:20
Unapomsaidia adui kwa moyo mkunjufu, unakuwa umejishusha kwa kiasi kikubwa sana kwakuwa katika uhitaji wake kwa hali ya kawaida ndio wakati mzuri wa kulipa kisasi. Tukikumbuka Daudi alivyojishusha kwa Sauli mara mbili hata asimuue, na Mungu alimbariki na kumuinua Daudi.
Kujishusha kunaghairi mabaya, hata kosa likasamehewa na kusahaulika. Abigaili alivyojishusha na kumuokoa mumewe Nabali asiuliwe na Daudi, hata Daudi akakubali ombi na kughairi uteketezaji aliokuwa amenuia nyumbani kwa Nabal.
1 Samweli 25:23 – 35
Kujishusha ni tabia ya Mungu ndani yetu, hivyo tunapojishusha tunasababisha watu waione nuru ya Mungu ikiwaangazia, ndio maana mtume Paulo alijishusha sana katika huduma yake. Kujishusha hakutizami tunapoteza mangapi katika mwili bali tunaweka hazina kiasi gani Mbinguni kwa Baba yetu.

No comments:

Post a Comment