Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Thursday, April 19, 2012

Kunuia Yaliyo Makuu



Ndoto ni kitu kizuri sana, hasa ndoto zenye kujenga na kutupa motisha. Wengi katika tulipokuwa wadogo tuliota maisha ya namna Fulani, ambayo ni mazuri sana yenye mafanikio bila kuwa na shida yoyote, lakini kuna usemi unasema ndoto huwa zinatimia walakini pia huwa hazitimii vile vile.

Kwanini huwa tunanuia au kupanga yaliyo makuu sana lakini inafikia wakati tunakata tamaa, hata kuona haiwezekani na kurudi nyuma? Tulipoupokea wokuvu tulikuwa na wito na moto wa hali ya juu sana katika kuitenda kazi ya Mungu, kusoma na kujifunza neno. Wengine tulinuia kuwa kama watumishi mbalimbali wakubwa duniani, lakini ile ari sasa imepotea, ule moto umefifia kama sio kuzima. Je, yale makuu tuliyonuia yameishia wapi?

Kunuia makuu ni jambo moja, na kufanikisha kile unachonuia ni chambo jingine tofauti kabisa kwani katika kufanikisha yale makuu tunayonuia siku zote lazima tulifuate na kulishika neno la Mungu linavyotuambia, vinginevyo hata tukitimiza nia zetu hazitakuwa za kudumu kwani hazina msingi wa kudumu.

Kuwatumikia wengine kunamuinua sana mtu siku zote, kama ambavyo Elisha alimtumikia Elia, hata akamwambia Elia kuwa si kwamba anataka tu kile alicho nacho ila anataka mara mbili zaidi ya roho iliyokuwa ndani ya yake. 2 Wafalme 2:9 – 14

Wenye uvumilivu siku zote katika Mungu hufika mbali sana hata kuona yale waliyonuia (ndoto zao) yakitimia kwa wakati ambao ni timilifu kwa Bwana Yesu, kama ambavyo Neno linasema kila kilicho kamili hutoka kwa Baba yetu wa Mianga. Yakobo 1:17

Tukimtizama Yusufu ambaye alikuwa akiota, lakini sio kwamba aliota tu ila aliamini na kuzishikilia ndoto zake hata zitimie, yamkini angekata tamaa mapema yote yasingewezekana kutimia, hata tunapotizama Yusufu aliteuliwa kuwa waziri mkuu wa Misri akiwa na miaka 30. Mwanzo 41: 39 – 46

Kung’ang’ania kulimfanya Jakobo akashindana na malaika, hata akabarikiwa, lakini pia mara zote Eliyah alipomuambia Elisha asimfuate maana Mungu amemtuma sehemu nyingine, Elisha alikamjibu kama Mungu aishivyo na roho yako iishivyo sitakuacha kamwe. 2 Wafalme 2: 1 – 2

Usipokata tamaa unajiweka kwenye nafasi ya kumshawishi Mungu afanye kitu siku zote, maana Daudi katika magumu yote aliyopitia hakukata tamaa, ingawa aliwindwa sana na Sauli ili amuue lakini katika yote Daudi alimkabidhi Mungu. 1 Samweli 26:17 – 24

Mapenzi ya Mungu yatimie siku zote katika maisha yetu. Maana, kama tunampenda Yesu, tutampenda na Baba pia, hivyo hatutaishi tukitenda mapenzi yetu ila daima mapenzi ya Baba yatimizwe maishani mwetu. Tukijaribu kulazimisha mambo kwa namna yetu ya akili na maarifa hakika tutakuwa tunapingana na makusudi ya Mungu katika maisha yetu. Mungu anahitaji tumuombe, tujifunze neno lake siku zote na tujinyenyekeze kwake. Yakobo 4:10

Sunday, April 8, 2012

Imani Timilifu


Ilimpasa Bwana wetu Yesu Kristo kupitia mateso yote hata kufa ili sisi tupate kupona pamoja na ukombozi mbali na dhambi, lakini si hilo tu ila tupate ushindi katika Yeye kwa kukishinda kifo alipofufuka siku ya tatu. Tufurahi kwani yeye ameshinda yote, hivyo nasi tunapokuwa ndani yake hakika tutashida.
Yohana 16:33

Leo tunakumbuka kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kiristo, lakini haitakuwa na maana sana kama huyu Yesu hafufuki pamoja nasi miyoyoni mwetu, haina faida kabisa. Mmoja wa wahalifu kati ya wale wawili aliosurubiwa naye pale msalabani alimtizama na kusema Bwana unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
Luka 23: 42 – 43

Imani ndani ya huyu mhalifu ilikuwa timilifu sana, maana walikuwa na Yesu msalabani, lakini bado aliamini kwamba hakika huyu ni Mungu mwenye uweza wote. Lakini katika upande mwingine tunaona jinsi Petro alivyomkana Yesu mara tatu kwa kukosa Imani, pia baada ya Yesu kufa wanafunzi wake walijifungia kwa hofu wakijua yote yameishia hapo.
Luka 24: 36 – 42

Inawezekana kabisa kwamba kama dada zake Lazaro ambao waliamini Yesu anaponya lakini walimuwekea mipaka katika kufufua, nasi pia inawezekana kabisa kwamba tunamfahamu Yesu na matendo yake ila Imani timilifu tunakosa, yamkini hata Imani kiasi cha chembe ya haradali tu ni shida. John 11: 17 – 25, 38 – 44.

Imani timilifu haiji hivi hivi ila ni kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, kwani yote yaliyo ya Imani ni yale ya rohoni ambayo hukua hata yakaonekana nje. Tunaona wanafunzi baada ya kujazwa na Roho Mtakatifu walitoka kwa ujasiri kwenda kuihubiri injili.
Matendo ya Mitume 2:14 – 17 

Tunapokumbuka kufufuka kwa Yesu Kristo, inatupasa tukumbuke pia kupokea ile ahadi aliyotuahidi ya Msaidizi ambaye ni Roho Mtakatifu, ambaye kwa huyo tutaweza kuitenda kazi katika shamba la Bwana, vinginevyo siku zote hatutaweza kwa kukosa Imani iliyo timilifu.
Waebrania 11:6

Imani timilifu ni kama ya Stefano aliyetolewa nje na kupigwa mawe bila kubadili msimamo, pia ni kama ya Paul na Sila waliofungwa gerezani bila kubadili msimamo, na Imani ya namna hii inapopita kwenye majaribu inakuwa na nguvu zaidi. Imani timilifu ni kuamini hata kama hatuoni muujiza, hata kama ni wagonjwa mahututi na zaidi sana hata kama tumepoteza kila kitu.

Dada mmoja mateka nyakati za vita vya dunia aliandika kwa kukwangua ukutani kabla hajafa “Naamini katika mwanga hata kama siuoni, naamini katika upendo hata kama siuhisi na ninaamini katika Mungu hata kama akikaa kimya”

2 Timotheo 2:13

Tuesday, April 3, 2012

Blessings on Obedience


28 “Now it shall come to pass, if you diligently obey the voice of the Lord your God, to observe carefully all His commandments which I command you today, that the Lord your God will set you high above all nations of the earth.
And all these blessings shall come upon you and overtake you, because you obey the voice of the Lord your God:
“Blessed shall you be in the city, and blessed shall you be in the country.
“Blessed shall be the fruit of your body, the produce of your ground and the increase of your herds, the increase of your cattle and the offspring of your flocks.
“Blessed shall be your basket and your kneading bowl.
“Blessed shall you be when you come in, and blessed shall you be when you go out.
“The Lord will cause your enemies who rise against you to be defeated before your face; they shall come out against you one way and flee before you seven ways.
“The Lord will command the blessing on you in your storehouses and in all to which you set your hand, and He will bless you in the land which the Lord your God is giving you.
“The Lord will establish you as a holy people to Himself, just as He has sworn to you, if you keep the commandments of the Lord your God and walk in His ways.
10 Then all peoples of the earth shall see that you are called by the name of the Lord, and they shall be afraid of you.
11 And the Lord will grant you plenty of goods, in the fruit of your body, in the increase of your livestock, and in the produce of your ground, in the land of which the Lord swore to your fathers to give you.
12 The Lord will open to you His good treasure, the heavens, to give the rain to your land in its season, and to bless all the work of your hand. You shall lend to many nations, but you shall not borrow.
13 And the Lord will make you the head and not the tail; you shall be above only, and not be beneath, if you heed the commandments of the Lord your God, which I command you today, and are careful to observe them.
14 So you shall not turn aside from any of the words which I command you this day, to the right or the left, to go after other gods to serve them.

Sahau Mabaya


Kuumizwa au kuumia ni hali ambayo ipo katika maisha yetu ya kila siku, na kwa namna moja au nyingine huwa tunajikuta tumeumia, lakini inatupasa kufahamu na kutambua kuwa mabaya yote huja kutoka kwa mwovu Ibilisi na Shetani ambaye kamwe hataki kutuona salama.

Mara nyingi tunapoumia tunashikwa na uchungu mwingi sana hasa aliyetuumiza anapokuwa ni ndugu au jamaa wa karibu sana. Haizuiliki kuwa na uchungu lakini hatutakiwi kuwa katika hali hiyo muda wote.
Zaburi 30:5b
Muhubiri 7:9

Inawezekana kabisa tumeshindwa na kuanguka katika mambo mengi sana ingawa tulifanya yote katika usahihi hata kujiuliza kama kweli Mungu yuko upande wetu? Baadhi yetu tumewekeza sana kwenye biashara, pengine elimu au hata ndugu zetu lakini malipo ni kinyume kabisa na jitihada. Yamkini hata tumepoteza ndugu wetu wa karibu sana tuliowapenda, tunaweza hata kumuuliza Mungu kwanini? Sisi hatujui, wala haina haja ya kuwa kwenye hali ya msongo wa mawazo ila ni kumuachia Mungu na kusonga mbele tena kwa Imani.
Mithali 3:5
Zaburi 50:15  

Kwa kujaribu kutumia akili, maarifa au hekima ya kibnadamu ndipo wengi sana tumepotea, hata ikafikia mahali tukajawa na hofu sana kiasi cha kupoteza maisha. Wangapi tunajua kuwa wapo wengi waliowaza sana kwa uchungu hata kukatisha maisha yao mapema?
Mithali 3:7 – 8 

Kama kungekuwa na watu wa kukata tamaa au kuishi kwenye uchungu pamoja na hasira maishani mwao basi ingekuwa Yusufu na Daudi, kwani walipata shida sana lakini Mungu aliacha yote haya akiwa na kusudi maalum katika maisha yao.
Isingekuwa uvumilivu Yusufu angekata tamaa na kujutia maisha yake, lakini mbali na kuvumilia kama angekuwa na uchungu pamoja na kisasi hakika angewarudi ndugu zake walipokwenda Misri.
Lakini pia Daudi angejawa na kisasi, hakika angemuua Sauli mara ya kwanza tu Mungu alipomuweka mikononi mwake, hasa wenzake walipomsihi ammalize au awaruhusu wao wammalize, lakini Daudi aliacha kusudi la Mungu litimie.
1 Samuel 24; 26

Siku zote, Mungu akishaweka hitimisho hatupaswi kabisa kuendelea kujiuliza na kukaa kwenye machungu na hasira kwakuwa kila siku ni mpya. Unapoishi na hasira au uchungu wa jana, tayari umeiharibu jana, unaiharibu na leo pia hata kesho.
Kutoka 3:14

Kuna usemi unasema “ Ni maamuzi yetu kuchagua kuishi kwenye uhuru wa kusamehe au gereza la uchungu”.