Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Tuesday, June 11, 2013

Kushindwa Unapokuwa Ni Ushindi


Katika maisha ya mwanadamu yoyote, maamuzi ni jambo la msingi sana tena la kuzingatia muda wote. Lakini maamuzi yanapofanyika kwa hekima na busara ya Mungu ili yawe sahihi, siku zote yanaleta matokeo ambayo ni sahihi na mazuri, maana sote tunaishi leo kutokana na maamuzi ambayo tuliyafanya jana, pia kesho kwa maamuzi tunayoyafanya leo.

Mtoto mdogo anapochukua uamuzi wa kujifunza kutembea, anaanza na hatua moja, ambayo itapelekea kupiga hatua ya pili hata ya tatu kabla hajadondoka. Ingawa kudondoka kunaonyesha hajatimiza lengo lakini bado hajashindwa ingawa kwa mwenzake anayetembea ataonekana kashindwa.

Daudi alipukuwa akikimbia ili kuokoa maisha yake toka mikononi mwa Sauli hakika alionekana ameshindwa kumkabili Sauli, hata ile hali ya ushujaa haikuonekana kwake. Zaidi hata mahali ambapo Daudi alipata fulsa mara mbili ya kuweza kumuua Sauli bila kufanya hivyo, hata wenzake naamini walimuona amekuwa dhaifu.
1 Samueli 24:5 – 7 | 1 Samueli 26:9 – 10

Kinachotuponza wengi ni kujihimu ili tuonekane kama wengine wanaotuzunguka, ili tupate umaarufu kuwa hakika tumeweza kukabiliana na mtu au jambo bila kujua kwamba tunajijengea utukufu na kujiinua ambapo si muda vitatuangamiza sisi wenyewe.
Yakobo 4:10 | Mithali 16:18

Daudi aliamua kufanya maamuzi yaliyo sahihi katika mpango wa Mungu, na hakika katika wakati uliostahiki akawa mfalme, maana hatimaye Mungu aliamua kati yake na Sauli.
Wafilisti walipofanikiwa kumkamata Samsoni, wakamng’oa macho waliamini kwamba hakika huo ndio mwisho wa nguvu zake, na kati ya mambo waliyofanikiwa kushinda hilo lilikuwa mojawapo maana Samsoni aliwasumbua sana.

Naamini Samsoni alifahamu jambo moja kwamba kushindwa kwake ni ushindi kwani kusudi la Mungu hakika lazima litimie, hata alipokuwa akisaga ngano nywele zake zikaanza kuota tena, akajua hakika kinachompasa ni kupiga hatua na kufanya maamuzi sahihi katika mpango wa Mungu, na hakika Samsoni akaua watu wengi zaidi wakati wa kifo chake kuliko hapo awali.
Waamuzi 16:23 – 30

Mungu ametukabidhi zana zote kuhakikisha kwamba tunashinda na kusudi lake linatimia, haijalishi tunatereza au kuanguka mara ngapi ila cha msingi ni maamuzi tuliyoamua na kunuia kuyafanya katika kusudi la Mungu ni lazima yatimie.

Inawezekana kabisa kuna nyakati tunakata tamaa, inawezekana nyakati fulani tunashindwa kuvumilia, lakini tumkumbuke Yusufu ambaye alivumilia na kusamehe yote ingawa ndugu zake waliona wameshammaliza hata ndoto zake hazitatimia.

Tumtizame pia Bwana wetu Yesu ambaye alinyenyekea hata mauti ya msalaba, hata akaonekana ameshindwa kabisa maana hakujinasua toka msalabani, lakini siku ya tatu alifufuka akiwa mshindi wa yote.

No comments:

Post a Comment