Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Tuesday, June 11, 2013

Roho Ya Heshima

Heshima ni kitu cha msingi sana katika maisha ya jamii, kiasi kwamba mahali penye heshima panatawaliwa na upendo pamoja na Amani.
Jamii tunayoishi imetawaliwa na dharau inayojengeka kutokana na mali, nafasi katika nyadhifa fulani pia elimu ambapo ni tofauti kabisa na mpango wa Mungu, kwani inatupasa kumheshimu kila mmoja haijalishi ni mkubwa au mdogo zaidi anacho au hana.
1 Timotheo 5:1 – 2
Mara nyingi tunakosa kubarikiwa kwa sababu ya jambo ambalo tunasema au kushabikia tukimkosea heshima ndugu, jamaa, mzazi na hata mtumishi wa Mungu kwakuwa tunaona yamkini kile alichokifanya si sahihi, ila jambo la msingi kukumbuka siku zote ni kwamba ile nafasi aliyonayo mhusika sisi hatujamuweka ila Mungu, na katika kumkosea heshima kwetu kitakachotupata ni laana.
Hesabu 12:1 – 14
Mambo mengi sana tunafanya au kusema tukiwakosea heshima wengine kwa kuiga au kufuata mkumbo wa wengine au jamii inasemaje, lakini tukumbuke kuwa katika mengi sana jamii huwa inakosea hivyo Neno la Mungu inabidi likae kwa wingi ndani yetu na kutuongoza siku zote.
Kutoka 20:12
Haijalishi mzazi ana kasoro ya namna gani, au anafanya makosa kiasi gani yamkini amekuwa mbaya kwako kwa mangapi lakini siku zote tunatakiwa kumheshimu na kumshukuru Mungu kwa yote. Kuwa na mzazi bado ni bahati sana maana wapo ambao hawana hata mmoja, zaidi tusipoweza kumheshimu mzazi tunayemuona haiwezekani kumheshimu Mungu tusiyemuona.
Mara nyingi sana tumesikia na kushuhudia yamkini nasi tumeshiriki kwa sehemu kuwasema vibaya viongozi wa ngazi fulani katika nchi yetu ikiwa ni pamoja na viongozi wa dini. Ikiwa kuna baya lolote au popote pale ambapo wamekosema, sio jukumu letu sisi kuwahukumu na kuwakosoa kwa namna ya kuwakosea heshima lah, ila siku zote hukumu ni juu ya Mungu kuwarekebisha yeye, sisi yatupata kuheshimu tukiitii mamlaka.
Daniel 3:8 – 30
Ingawa Shedrack, Meshack and Abed-Nego walimwabudu Mungu wa kweli, pia ilikuwa haki kwako  kutokuanguka na kuisujudia sanamu ya mfalme Nebuchadnezzer, hata hivyo walitunza heshima yao juu ya mfalme kwa jinsi walivyomjibu kabla pia baada ya kuingizwa kwenye tanuru la moto lilikokuwa limechochewa mara saba zaidi.
Tumuombe sana Mungu wetu atujengee roho ya heshima ndani yetu, zaidi heshima ni kitu cha bure ambacho hakikugharimu unapokitoa zaidi unapata akiba ya Baraka ambapo kwa wakati Mungu anakuinua. Wenye roho ya heshima wanafika mbali sana katika maisha wakimuona Mungu akitenda mambo makuu na kuwapigania sana.

No comments:

Post a Comment