Pages

Nataka Kuokoka Sasa Hivi!

Ndugu yangu, hakuna kilicho bora sana duniani na baada ya maisha haya zaidi ya roho yako? Je, unafahamu baada ya maisha ya hapa duniani kuna maisha mengine ambayo wewe una maamuzi ya asilimia mia kuchagua?
Fahamu kuwa kuna Mbingu na Jehanamu. Mshahara wa dhambi daima ni mauti, na mshahara wa mema ni uzima wa milele. Chagua uzima ukaishi milele kwakuwa maisha ya hapa duniani ni ya kitambo kifupi sana nayo yamejaa masumbuko na taabu nyingi sana kila inapoitwa leo.
Yesu anakupenda sana, inawezekana kuna mtu anakupenda sana ila Yesu anakupenda zaidi ya wote duniani hivyo nakushauri ukate shauri umfuate yeye maana atakupa kustarehe milele na kuurithi ufalme wa mbinguni pamoja naye.

Thursday, June 13, 2013

Furaha Huja Asubuhi


Kuiona siku nyingine mpya ni upendeleo, zaidi ni baraka ya pekee sana kutoka kwa Mungu wetu ingawa kwa wengi wetu hatujui uthamani wa kuiona tena siku nyingine ila inakuwa ni kawaida tu au mazoea yasiyobeba uzito wowote.
Mungu wetu ametujalia furaha ya kuwa nayo siku zote na wakati wote, ingawa muda mwingi na katika mambo mengi tunachagua kuwa na hofu tukihuzunika sana. Jambo moja la msingi kukumbuka siku zote ni kwamba kinachotutenganisha sisi na furaha ni kutokulijua Neno la Mungu, maana Neno linatuambia wazi majonzi hudumu usiku lakini furaha huja asubuhi.
Zaburi 30:5

KInachotuumiza ni kwakuwa tunaamua kuhangaikia sana vile ambayo havitakiwi kuhangaikiwa, pia hatujui namna ya kuthamanisha vile tulivyonavyo tukishukuru na kumtukuza Mungu, ndio maana siku zote tunajiona sisi ni wahitaji tu, zaidi haijawahi kufikia siku tukatosheka.
Mathayo 6:25 – 34 | 1 Timotheo 6:6 – 10
Wengi tunajawa na hasira pamoja na uchungu kutokana na matukio mbali mbali yanayotukuta kwenye maisha yetu ya kila siku, pia hatuwezi kuizuia hasira kutufika wala uchungu lakini hatutakiwi kuviruhusu vitutawale maishani mwetu. Hata kwenye msiba wanaomboleza kwa muda, lakini wakiendelea kuomboleza siku zote ina maana wameamua kubadili mfumo wa maisha Mungu aliouweka kabisa. Tunapoishi kwa maumivu ya jana au siku za nyuma ina maana tumeamua kuikataa leo.
Zaburi 118:24
Mtumishi wa Mungu Daudi alilitambua kwamba kila siku ni mpya, na inampasa kushangilia na kushukuru katika hiyo. Nasi inatupasa kubadili namna ya maisha yetu, tukubali kwa yote yaliyopita hakika hatuwezi kuyabadilisha ila tunaweza kuanza sasa na kufanya yaliyo mema zaidi mbele za Mungu na jirani zetu.
Tunapoikataa furaha asubuhi tunampa shetani nafasi kuiteka siku yetu, ndio maana kuna watu wanasema wameamka vibaya ingawa hawaumwi ila anakuwa na hasira tu siku nzima wala hajisikii kufanya kitu chochote. Cha msingi cha kufahamu ni kwamba furaha ni chaguo kama ambavyo huzuni pia ni chaguo la mtu binafsi. Ndio maana Joshua aliwaambia wana wa Israeli wachague ni nani watakayemtumikia ila yeye na nyumba yake wanamtumikia Bwana.
Joshua 24:15
Tunapoamka asubuhi tunatizama nini? Tunakumbuka jana ilikuwa mbaya kiasi gani, tunatizama ni vingapi ambavyo tunahitaji lakini hatuna au tunatizama jinsi ambavyo hatuko kama wengine? Haya yote tunapoyatizama yanatuletea huzuni siku nzima, lakini tukiangalia uhalisia wa kwamba ni siku nyingine mpya, tukamshukuru Mungu kwa uzima na afya njema, tukaona taswira ya Mungu ndani yetu, na kujua kuwa Mungu yupo kazini kutubariki, kututetea, kutupigania na kutuongoza; hakika hatutakuwa na muda wa kuikumbatia huzuni na hasira.
Furaha ni hali inayokosekana kwa watu wengi sana, hata tunakosa amani moyoni pengine hata kukata tamaa ya maisha kabisa. Siri moja ya msingi, inatakiwa tufurahie kwanza vile tulivyonavyo, zaidi sana jinsi tulivyo ndipo tutasababisha Mungu atubariki kwa vingine vingi zaidi.

No comments:

Post a Comment